Friday, September 4, 2015

Watanzania wametakiwa kutafakari kwa kina mustakabali wa taifa katika wakati huu wa uchaguzi



 Watanzania hususani vijana wametakiwa kukaa na kutafakari kwa kina mustakabali wa taifa letu katika wakati huu wa uchaguzi na kuchagua viongozi ambao hawatakuwa vibaraka wa mataifa mengine kutokana na Tanzania kuwa na maliasili nyingi ikiwemo gesi na mafuta ambayo huenda mataifa hayo yakautumia uchaguzi huu kuwaweka madarakani vibaraka wao na kuifanya Tanzania kuwa muhanga wa maliasli zake kwa kushindwa kufikia malengo ya kuwaondolea umasikini watanzania.
Hayo yamesemwa na mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi CCM Dr John Pombe Magufuli wakati akizungumza na viongozi wa ngazi za juu wa jumuia ya wazazi Tanzania ambapo kupitia kwao amewataka kuwaelimisha vijana juu ya kufanya mabadiliko ya pupa bila kujali athari za kesho kwa kuwa mjuto ni mjukuu.
 
Aidha Dr Magufuli ameendelea kusisitiza suala la kutunzwa kwa amani ya Tanzania na kwamba watanzania wasikubali kufarakanishwa kutokana na itikadi ya vyama vyao na kuwataka kumwamini kuwa ana uwezo wa kuleta mabadiliko ya kimfumo ndani ya chama cha mapinduzi na serikali kwa ujumla kama china ilivyofanya badala ya kufanya mabadiliko ya jazba kama nchi za Libya.
 
Mwenyeikiti wa jumuia ya wazazi wa chama cha mapinduzi Alhaji Abdala Bulembo amwakikishia mgombea huyo kuwa jumuia imejipanga kumsemea ili aendelee kuaminiwa na watanzania kwani kazi alizozifanya zinaeleweka na kuheshimiwa na watanania.

No comments:

Post a Comment