Saturday, August 22, 2015

MGOMBEA UDIWANI WA CCM APIGWA RISASI HUKO MWANZA


Mgombea Udiwani wa Chama cha Mapinduzi kata ya Sangabuye Mwanza, James Katole amejeruhiwa na risasi na watu wasiofahamika.

Mgomgea huyo alipigwa risasi juzi akiwa kijijini kwake Nyangoka, Busega ambapo alikwenda kuwasalimia wazazi wake.

Katole alisema alikua nje ya nyumba yao majira ya saa 1 usiku akiwa na wazazi wake gafla walikuja watu ambao hawafahamu na alipowahoji ni kina nani hawakuzungumza lolote zaidi kukaa kimya.

‘Walikuwa wamevaa makoti meusi, nilipowauliza shida yao hawakusema loloyte nikaamua kuwafuata ndipo walipofyatua risasi ambayo ilinipata kwenye kidole na kumpiga mama yangu ubavuni na kutokea upande wa pili’ Katole.

Alisema watu hao ambao hawakuchukua kitu chochote baada ya tukio hilo waliondoka huku wakitembea kawadia na kutokomea gizani.
Via>>>Eddy Blog

No comments:

Post a Comment